Al Shabab yapiga marufuku bidhaa za Uturuki
Kundi la wanamgambo wa Al Shabab limepiga marufuku uuzaji na ununuzi wa bidhaa zilizoundwa Uturuki nchini Somalia.
Al-Shabab
imewaarifu wafanyibiashara katika majimbo ya Kusini mwa Somalia na
maeneo ya Lower Shabelle kuwa bidhaa zinazotokea Uturuku ni haramu.Jarida linalochapishwa kwenye tovuti ya Falaar inasema kuwa wale watakaokiuka amri hiyo ''watachomwa moto wakiwa hai''
Wafanyibiashara katika maeneo yaliyoathirika tayari wamelalamika kuwa amri hiyo itawaathiri vibaya.
Al-Shabab inasema kuwa imechukua hatua hiyo kwani Uturuki inasaidia mahasidi wao serikali ya Somalia.
No comments:
Post a Comment