Tikiti maji ni mboga/tunda linalolimwa
hasa katika maeneo ya joto lenye kiwango cha joto cha 22-28 0c na mvua 600 -
400mm kwa mwaka.
Matikiti yanahitaji hali ya hewa yenye
joto na mwangaza wa jua wa kutosha . Kiwango kidogo cha unyevu kwa sababu
unyevu mwingi unasababisha maradhi.
Unyevunyevu mwingi unaadhiri
ubora na utamu wa tunda. Vilevile, yanastawi vizuri katika aina mbalimbali za
udongo wenye rotuba ya kutosha na
wenye kupitisha maji vizuri.
Aina
za matikiti maji
NEGRA F1
Aina hii ya matikiti maji ni ya mviringo yenye mazao na sifa nzuri”
Ubora wake
• Yana mazao mazuri, na uwezo wa kukupa tani
46 kwa kila ekari
• Ni matamu sana na yenye wekundu wa
kung’ara
• yanakomaa katika muda wa siku 100-120
• Ni mviringo na yenye rangi ya kijani
kibichi na hutoa matunda yenye mizani
kati ya kilo 7-10
• Mmea hukua haraka na una mazao mazuri
•Yamezungukwa na nyama ngumu, nzuri, yenye
kukuwezesha kusafirisha hadi sehemu za
mbali
• Yana kinga dhidi ya ugonjwa wa mnyauko unaosababishwa na vimelea aina ya Fusari (Fusarium wilt)
SENTINEL F1
ni aina mpya ya matikiti ya mviringo marefu”
Ubora wake
• yanaweza kuzaa sana hadi tani 50 kwa
kila ekari
• Ni marefu, yameshiba na yana rangi ya
pundamilia
• ni tamu, yan wekundu uliokolea na nyama
iliyo na maji mengi
• Yanawezakutoa matunda ya kufanana na yaliyo
na uzani kati kilo 11 - 14
• Matunda yana nyama nyingi na umbo
inayokuwezesha kusafirisha masafa marefu
• yana kinga dhidi ya maradhi ya vimelea aina
ya Fusari (Fusarium wilt Race 1)
• yanakua tayari katika muda wa siku 100
-120
Mbali na kuwa na faida mbali mbali
kiafya tikiti maji linaweza kumtoa mkulima wa kawaida katika umaskini. Hii
kutokana na sababu zifuatazo.
·
Tikitimaji ni zao la bustani linalochukua miezi 3-4 kuvunwa, hivyo kwa
mwaka linaweza kuvunwa mara 3 hadi 4
·
kwa ekari moja mavuno ya tikiti
maji ni matunda 2000 - 8000 au zaidi kwa miezi 3-4 kutokanana uangalizi
wa mkulima katika shamba ikiwa ni kutumia mbolea kama inavyo takiwa, kuzuia
wadudu na magonjwa, n.k. Pamoja na nafasi iliyotumika katika upandaji (1x1m,
2x2m, 1.5 x 1.5m).
JINSI YA KUJUA FAIDA
Katika maeneo mengi ya Tanzania bei ya
tikiti maji lenye sifa nzuri ni shilingi 2,000/= hadi 3,000/=
kwa bei ya 2,000/= na mavuno ya 2000
matunda/ekari (Matunda mazuri)
Baada ya mavuno utajipatia kiwango cha
chini kisichopungua jumla ya Tsh.4,000,000/= kwa mwaka ni 12,000,000/= kwa
mavuno ya mara tatu kwa mwaka kwa ekari.
Gharama hii itaenda juu zaidi ama itapungua kutegemea na idadi ya matunda uliyoyapata katika ekari mmoja na bei ya muuzaji. Hivyo unaweza ukapata faida kubwa zaidi ukiongeza uangalizi wa shamba lako na kufuata utaratibu katika ulimaji wa zao hili.
MAHITAJI
Tikiti maji linahitaji mbolea, maji,
kemikali za kuua wadudu na magonjwa pamoja na maandalizi mabali mbali ya shamba
ambavyo gharama yake haizidi Tsh. 500,000/= katika uangalizi mkubwa
FAIDA
Hivyo mkulima katika uangalizi wa mzuri
ana uhakika wa kupata faida ya Tsh. 3,500,000/= na zaidi kila baada ya
miezi 3-4.
Ushauri: Kwa mafanikio mazuri na kuinuana kiuchumi wakulima
wakiungana na kufanya kilimo bishara watakuwa na nafasi kubwa ya
mafanikio kwa maana kiuchumi wanataweza kusaidiana ili kuinua mtaji na
kuweza kupata kiasi cha kuanzia shughuli zao za kilimo.
Nmeelewa somo
ReplyDeleteThanx brother yaaan ufafanuzi wako ni Wa hali ya juu ..binafsi nashukuru kwa muongozo ..naitaji kuanza hii biashara mwakani mwezi wq tatu mungu akijaalia....ila no bado mwanafunzi Wa chuo na shamba langu liko mbali na ninapoishi ..sasa ninahofi uangalizi niahauri juu ya hili please.....pia tungependa muongozo juu ya a in a gani ya dawa tutumie kwa magonjwa yap pleaseeee
ReplyDeleteThx kwa ushauri mimi ndo nataka nianze vandalize ya,shamba this week ningependa kujua ni maandalizi gani natakiwa nifanye na yanachukua mda gani na jee naweza andaa shamba na kupanda ndani ya week moja?
ReplyDeleteNa ni mbolea gani na kiasi gani inayotakiwa?
Be blessed my brother, ushauri wako ni wakueleweka Kansas. Mungu akutangulie uzidi kutupa somo la kujenga jamii.
ReplyDeleteasante kwa ufafanuz huo, ila samahan je nikitaka kukodisha shamba inagharimu shng ngap
ReplyDeleteLinu, bei ya kukodi shamba inategemea na mahali unapotaka kuweka shamba lako. bei zinatofautiana kati ya sehemu na sehemu. Suala la msingi ni kubaini eneo ambalo lina vigezo muhimu kwa ajili ya kilimo cha zao hili. Kwa mfano,, ukienda Ifakara na ukanda wote wa chini kule utapata bei nyingine nzuri tu kama 50,000/- kwa msimu ila sasa cha msingi ni je, mazingira ya kule yana favour kilimo cha zao hili? tafuta na fuatilia. sehemu nyingine ni Wangingombe, kule ni kuzuri sana ila ni lazima ukaongee na serikali za vijiji vya kule ili ujue mipango yao na ada ambazo kijiji imeziweka na ndizo utakazotumia kukodisha shamba... In general andaa kama 50,000/- hadi 70,000/- kwa ajili ya ukodishaji mashamba kwa ekari moja kwa msimu.... hii ni kwa maeneo mengi hapa nchini.
ReplyDeleteiko poa saana
ReplyDeleteSana mkuu yani tutakuwa pamoja sana manake Mimi tayari nimeshaandaa shamba nategemea kupanda tu na ninaomba unielekeze mbolea inayotumika wakati was kupanda
ReplyDeleteTumia D.A.P
DeleteSana mkuu yani tutakuwa pamoja sana manake Mimi tayari nimeshaandaa shamba nategemea kupanda tu na ninaomba unielekeze mbolea inayotumika wakati was kupanda
ReplyDeletenimependa sana ulivyoelezea kiongozi,safi sana we ni mwalim mzuri
ReplyDelete