Polisi nchini Ubelgiji wanamsaka
mshukiwa anayedaiwa kuhusika katika mashambulio yaliyotekelezwa mjini
Brussels Jumanne na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 30.
Mwanamume huyo alionekana akitembea pamoja na washukiwa wengine wawili uwanja wa ndege wa Zaventem
kabla ya milipuko miwili kutokea.Washukiwa wenzake wawili walifariki katika mashambulio hayo baada ya kujilipua, mwendesha mashtaka wa Ubelgiji amesema.
Misako ya kuwasaka magaidi imefanywa maeneo mbalimbali Ubelgiji.
Kundi linalojiita Islamic State (IS) limedai kuhusika.
Taarifa iliyopakiwa mtandaoni na kundi hilo ilisema maeneo hayo yaliyoshambuliwa “yaliteuliwa kwa umakinifu mkubwa” na kuonya kuwa kutatokea mabaya zaidi kwa mataifa yanayopinga kundi la Islamic State.
No comments:
Post a Comment