Friday, March 25, 2016

Watumishi watatu wa Halmashauri ya Bariadi-Simiyu kwa tuhuma mbali mbali



Serikali wilayani Bariadi Mkoani Simiyu imewasimamisha kazi Watumishi watatu wa Halmashauri ya Bariadi kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo ya walimu kuuziwa vitambulisho vya kazi,fomu ya (OPRAS) na walimu 22 waliosimamishwa na  kurudishwa kazini na kushindwa kulipwa madai yao ya miaka mitatu kiasi cha milioni 150 baada ya kuagizwa na Tume  ya walimu TSD na kukaidi kufanya hivyo.
 
Uamuzi wa kuwasimamisha kazi Watumishi hao umekuja muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao cha pamoja kati ya Mkuu wa Wilaya hiyo Ponsiano Nyami  na waalimu zaidi ya elfu moja wa Wilaya ya Bariadi kilichofanyika katika Ukumbi wa Bariadi Motel ambapo walipomueleza mkuu huyo namna wanavyonyanyasika na watumishi hao  kiasi cha kukata tamaa,ya kufundisha kutokana na  madai yao yakiwemo malimbikizo ya mishahara.
 
 
Mara baada ya kikao hicho Mkuu wa Wilaya akaitisha kikao cha dharura  cha Kamati ya Ulinzi na Usalama,ambapo akatoa  kauli ya Serikali ya kuwasiamamisha Watumishi hao mbele ya waandishi wa habari.
 
Sambamba na kuwasimamisha Watumishi hao pia ameviagiza Vyombo Dola ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kuhakikisha wanachunguza tuhuma zote zinazowakabili,huku akimuagiza Mkuu wa Polisi wa Wilaya  kuwakamata na kuwafikisha ahakamani wale wenye maduka ya vifaa vya shule ambao wamekuwa wakiuza za fomu za OPRAS ambazo ni za serikali katika maduka yao

No comments:

Post a Comment